Deuteronomy 33:1-6

Musa Anayabariki Makabila

1 aHii ndiyo baraka Musa mtu wa Mungu aliyotamka kwa Waisraeli kabla ya kifo chake. 2 bAlisema: Bwana alikuja kutoka Mlima Sinai,
akachomoza kama jua juu yao
kutoka Mlima Seiri,
akaangaza kutoka Mlima Parani.
Alikuja pamoja na watakatifu makumi elfu
kutoka kusini,
kutoka materemko ya mlima wake.

3 cHakika ni wewe ambaye huwapenda watu,
watakatifu wako wote wamo mkononi mwako.
Miguuni pako wote wanasujudu
na kutoka kwako wanapokea mafundisho,

4 dsheria ile Musa aliyotupa sisi,
tulio milki ya kusanyiko la Yakobo.

5 eAlikuwa mfalme juu ya Yeshuruni
Yeshuruni maana yake ni Yeye aliye mnyofu, yaani Israeli.

wakati viongozi wa watu walipokusanyika,
pamoja na makabila ya Israeli.


6 g“Reubeni na aishi, asife,
wala watu wake wasiwe wachache.”

Copyright information for SwhKC