Proverbs 17:1-6
1 aAfadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivukuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 bMtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye,
naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 cKalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,
bali Bwana huujaribu moyo.
4 Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya;
mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 dYeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake;
yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 eWana wa wana ni taji la wazee,
nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
Copyright information for
SwhKC