Proverbs 8:22-27


22 aBwana aliniumba mwanzoni mwa kazi yake,
kabla ya matendo yake ya zamani;

23 bniliteuliwa tangu milele,
tangu mwanzoni, kabla ya dunia kuumbwa.

24 cWakati hazijakuwepo bahari, nilikwishazaliwa,
wakati hazijakuwepo chemchemi zilizojaa maji;

25 dkabla milima haijawekwa mahali pake,
kabla vilima havijakuwepo, nilikwishazaliwa,

26 ekabla hajaumba dunia wala mashamba yake
au vumbi lolote la dunia.

27 fNilikuwepo alipoziweka mbingu mahali pake,
wakati alichora mstari wa upeo wa macho
juu ya uso wa kilindi,
Copyright information for SwhKC