Psalms 18:1-6

Wimbo Wa Daudi Wa Ushindi

(2 Samweli 22:1-51)

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi Mtumishi Wa Bwana Aliyomwimbia Bwana Wakati Bwana Alipomwokoa Mikononi Mwa Adui Zake Wote, Na Pia Mkononi Mwa Sauli)


1 aNakupenda wewe, Ee Bwana,
nguvu yangu.


2 b Bwana ni mwamba wangu,
ngome yangu na mwokozi wangu,
Mungu wangu ni mwamba,
ambaye kwake ninakimbilia.
Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu,
ngome yangu.

3 cNinamwita Bwana anayestahili kusifiwa,
nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.


4 dKamba za mauti zilinizunguka,
mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

5 eKamba za kuzimu zilinizunguka,
mitego ya mauti ilinikabili.

6 fKatika shida yangu nalimwita Bwana,
nilimlilia Mungu wangu anisaidie.
Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu,
kilio changu kikafika mbele zake,
masikioni mwake.

Copyright information for SwhKC