Psalms 34:1-6

Sifa Na Wema Wa Mungu

(Zaburi Ya Daudi, Alipojifanya Mwendawazimu Mbele Ya Abimeleki, Ambaye Alimfukuza, Naye Akaondoka)


1
Zaburi hii imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.
bNitamtukuza Bwana nyakati zote,
sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.

2 cNafsi yangu itajisifu katika Bwana,
walioonewa watasikia na wafurahi.

3 dMtukuzeni Bwana pamoja nami,
naam, na tulitukuze jina lake pamoja.


4 eNilimtafuta Bwana naye akanijibu,
akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

5 fWale wamtazamao hutiwa nuru,
nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.

6 gMaskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia,
akamwokoa katika taabu zake zote.
Copyright information for SwhKC