c Za 14:7; 53:6; 85:1; 126:4; Yer 30:18; 33:11; Eze 16:53; Yoe 3:1; Sef 2:7; Kum 13:17; Mwa 48:21; 11:4; Kum 4:27; Isa 11:11; Yer 12:15; 16:15; 26:4; Yer 29:14; 48:47; 49:6
Deuteronomy 30:1-6
Mafanikio Baada Ya Kumgeukia Bwana
1 aWakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mwenyezi Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa, 2 bhapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mwenyezi Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo, 3 cndipo Bwana Mwenyezi Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya. 4 dHata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mwenyezi Mungu wako atakukusanya na kukurudisha. 5 eYeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako. 6 f Bwana Mwenyezi Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi.
Copyright information for
SwhKC