Genesis 11:10-15

10 aHivi ndivyo vizazi vya Shemu.

Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
11Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

12 bWakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela. 13Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

14Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi. 15Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

Copyright information for SwhKC