Isaiah 57:1-2

Ibada Ya Sanamu Ya Israeli Iliyo Batili


1 aMwenye haki hupotea,
wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake;
watu wanaomcha Mungu huondolewa,
wala hakuna hata mmoja anayeelewa
kuwa wenye haki wameondolewa
ili wasipatikane na maovu.

2 bWale waendao kwa unyofu
huwa na amani;
hupata pumziko walalapo mautini.

Copyright information for SwhKC