Proverbs 7:1-6
Onyo Dhidi Ya Mwanamke Mzinzi
1 aMwanangu, shika maneno yangu
na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
2 bShika amri zangu nawe utaishi;
linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3 cYafunge katika vidole vyako;
yaandike katika kibao cha moyo wako.
4 Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”
uite ufahamu jamaa yako;
5 dwatakuepusha na mwanamke mzinzi,
kutokana na mwanamke mpotovu
na maneno yake ya kubembeleza.
6 Kwenye dirisha la nyumba yangu
nilitazama nje kupitia upenyo
kwenye mwimo wa dirisha.
Copyright information for
SwhKC