Psalms 59:1-6

Kuomba Ulinzi Wa Mungu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Usiharibu. Utenzi Wa Daudi. Wakati Sauli Alipotuma Wapelelezi Nyumbani Mwa Daudi Ili Wamuue)


1 a bEe Mungu, uniokoe na adui zangu,
unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.

2 cUniponye na watu watendao mabaya,
uniokoe kutokana na wamwagao damu.


3 dTazama wanavyonivizia!
Watu wakali wananifanyia hila,
ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea
wala kutenda dhambi.

4 eSijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia.
Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!

5 fEe Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli!
Zinduka uyaadhibu mataifa yote,
usionyeshe huruma kwa wasaliti.


6 gHurudi wakati wa jioni,
wakibweka kama mbwa,
wakiuzurura mji.
Copyright information for SwhKC