Psalms 72:6-11


6 aAtakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa,
kama manyunyu yanyeshayo ardhi.

7 bKatika siku zake wenye haki watastawi;
mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.


8 cAtatawala kutoka bahari hadi bahari
na kutoka Mto
Yaani Mto Frati.
mpaka miisho ya dunia.

9 Makabila ya jangwani watamsujudia,
na adui zake wataramba mavumbi.

10 eWafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali
watamletea kodi;
wafalme wa Sheba na Seba
watampa zawadi.

11 fWafalme wote watamsujudia
na mataifa yote yatamtumikia.

Copyright information for SwhKC