Matthew 1
Kumbukumbu Za Ukoo Wa Yesu Kristo
1Habari za ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Abrahamu:2Abrahamu akamzaa Isaki,
- Isaki akamzaa Yakobo,
- Yakobo akamzaa Yuda na ndugu zake,
- Solomoni akamzaa Rehoboamu,
- Rehoboamu akamzaa Abiya,
- Abiya akamzaa Asa,
- Yekonia alimzaa Shealtieli,
- Shealtieli akamzaa Zerubabeli,
Kuzaliwa Kwa Yesu Kristo
18Basi Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama yake alikuwa ameposwa na Yosefu, lakini kabla hawajakutana kimwili, Maria alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 19Kwa kuwa Yosefu, mwanaume aliyekuwa amemposa alikuwa mtu mwadilifu, hakutaka kumwaibisha Maria hadharani, aliazimu kumwacha kwa siri.20Lakini mara alipoazimu kufanya jambo hili, malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto na kusema, “Yosefu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, kwa maana mimba aliyo nayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 21Naye atamzaa mwana, nawe utamwita Jina lake Yesu ▼
▼1:21 Yesu ni Kiyunani, kwa Kiebrania ni Yoshua au Yeshua, maana yake ni Yehova ni wokovu
, kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao.”22Haya yote yametukia ili litimie lile Bwana alilokuwa amenena kupitia nabii, akisema: 23“Tazama, bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita Jina lake Imanueli,” maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
24Yosefu alipoamka kutoka usingizini, akafanya kama vile alivyoagizwa na malaika wa Bwana, akamchukua Maria kuwa mke wake. 25Lakini hawakukutana kimwili mpaka Maria alipojifungua mwanawe kifungua mimba akamwita Jina lake Yesu.
Copyright information for
Neno