1 Chronicles 16:8-13


8 aMshukuruni Bwana, liitieni jina lake;
wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

9 bMwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa;
waambieni matendo yake yote ya ajabu.

10 cLishangilieni jina lake takatifu;
mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.

11 dMtafuteni Bwana na nguvu zake;
utafuteni uso wake siku zote.

12 eKumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,
miujiza yake na hukumu alizozitamka,

13 enyi wazao wa Israeli mtumishi wake,
enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

Copyright information for SwhKC