1 Corinthians 9:1-6

Haki Za Mtume

1 aJe, mimi si huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Isa, Bwana wetu? Je, ninyi si matunda ya kazi yangu katika Bwana? 2 bHata kama mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu, kwa maana ninyi ni mhuri wa utume wangu katika Bwana.

3Huu ndio utetezi wangu kwa hao wanaokaa kunihukumu. 4 cJe, hatuna haki ya kula na kunywa? 5 dJe, hatuna haki ya kusafiri na mke anayeamini, kama wanavyofanya mitume wengine na ndugu zake Bwana na Kefa?
Yaani Petro.
6 fAu ni mimi na Barnaba tu inatubidi kufanya kazi ili tuweze kupata mahitaji yetu?

Copyright information for SwhKC