2 Samuel 22:2-7

2 aAkasema: Bwana ni mwamba wangu,
ngome yangu na mwokozi wangu,

3 bMungu wangu ni mwamba wangu,
ambaye kwake ninakimbilia,
ngao yangu na pembe ya wokovu wangu.
Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu
na mwokozi wangu,
huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.

4 cNinamwita Bwana, anayestahili kusifiwa,
nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.


5 d“Mawimbi ya mauti yalinizunguka,
mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

6 eKamba za kuzimu
Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, maana yake ni Shimo lisilo na mwisho.
zilinizunguka,
mitego ya mauti ilinikabili.

7 gKatika shida yangu nalimwita Bwana,
nilimlilia Mungu wangu.
Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu,
kilio changu kikafika masikioni mwake.

Copyright information for SwhKC