Acts 9:1-6

Kuokoka Kwa Sauli

(Matendo 22:6-16; 26:12-18)

1 aWakati ule ule, Sauli alikuwa bado anazidisha vitisho vya kuua wanafunzi wa Bwana, akamwendea kuhani mkuu, 2 bnaye akamwomba kuhani mkuu ampe barua za kwenda kwenye masinagogi huko Dameski, ili akimkuta mtu yeyote wa Njia Ile, akiwa mwanaume au mwanamke, aweze kuwafunga na kuwaleta Yerusalemu. 3 cBasi akiwa katika safari yake, alipokaribia Dameski, ghafula nuru kutoka mbinguni ikamwangaza kotekote. 4 dAkaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, “Sauli, Sauli, mbona unanitesa?”

5 eSauli akajibu, “U nani wewe, Bwana?”

Ile sauti ikajibu, “Mimi ni Isa unayemtesa.”
6 f“Sasa inuka uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.”

Copyright information for SwhKC