a Hes 21:17; Amu 5:3; 2Sam 22:1; 1Nya 16:9; Ay 36:24; Za 59:16; 105:2; Ufu 15:3; Za 13:6; 21:13; 27:6; 61:8; 104:33; 106:12; Isa 12:5-6; 42:10; 44:23; Kum 11:4; Za 76:6; Yer 51:21; Kut 14:27; Yn 2:11
Exodus 15:1-6
Wimbo Wa Musa Na Miriamu
1 aNdipo Musa na Waisraeli wakamwimbia Bwana wimbo huu: “Nitamwimbia Bwana,kwa kuwa ametukuzwa sana.
Farasi na mpanda farasi
amewatosa baharini.
2 b Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu;
amekuwa wokovu wangu.
Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu,
Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.
3 c Bwana ni shujaa wa vita;
Bwana ndilo jina lake.
4 dMagari ya vita ya Farao na jeshi lake
amewatosa baharini.
Maafisa wa Farao walio bora sana
wamezamishwa katika Bahari ya Shamu.
5 eMaji yenye kina yamewafunika,
wamezama mpaka vilindini kama jiwe.
6 f“Mkono wako wa kuume, Ee Bwana
ulitukuka kwa uweza.
Mkono wako wa kuume, Ee Bwana,
ukamponda adui.
Copyright information for
SwhKC