Genesis 25:1-6

Kifo Cha Ibrahimu

1Ibrahimu alioa mke mwingine, ambaye jina lake aliitwa Ketura. 2 aHuyu alimzalia Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua. 3Yokshani alikuwa baba wa Sheba na Dedani, wazao wa Dedani walikuwa Waashuri, Waletushi na Waleumi. 4 bWana wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Eldaa. Hawa wote walikuwa uzao wa Ketura.

5 cIbrahimu akamwachia Isaka kila kitu alichokuwa nacho. 6 dLakini Ibrahimu alipokuwa bado hai, akawapa watoto wa masuria wake zawadi, kisha akawaondoa waende kuishi pande za mashariki mbali na mwanawe Isaka.

Copyright information for SwhKC