Hosea 8:1-6

Israeli Kuvuna Kisulisuli


1 a“Wekeni tarumbeta midomoni mwenu!
Tai yuko juu ya nyumba ya Bwana
kwa sababu watu wamevunja Agano langu,
wameasi dhidi ya sheria yangu.

2 bIsraeli ananililia,
‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’

3 cLakini Israeli amekataa lile lililo jema,
adui atamfuatia.

4 dWanaweka wafalme bila idhini yangu,
wamechagua wakuu bila kibali changu.
Kwa fedha zao na dhahabu
wamejitengenezea sanamu kwa ajili
ya maangamizi yao wenyewe.

5 eEe Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama!
Hasira yangu inawaka dhidi yao.
Watakuwa najisi mpaka lini?

6 fZimetoka katika Israeli!
Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu.
Atavunjwa vipande vipande,
yule ndama wa Samaria.

Copyright information for SwhKC