Isaiah 12:1-3

Kushukuru Na Kusifu

1 aKatika siku ile utasema: “Nitakusifu wewe, Ee Bwana.
Ingawa ulinikasirikia,
hasira yako imegeukia mbali
nawe umenifariji.

2 bHakika Mungu ni wokovu wangu;
nitamtumaini wala sitaogopa.
Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu;
amekuwa wokovu wangu.”

3 cKwa furaha mtachota maji
kutoka visima vya wokovu.

Copyright information for SwhKC