Isaiah 8:1-6
Ashuru, Chombo Cha Bwana
1 a Bwana akaniambia, “Chukua gombo kubwa, uandike juu yake kwa kalamu ya kawaida jina: Maher-Shalal-Hash-Bazi. ▼▼ Maher-Shalal-Hash-Bazi maana yake ni Haraka kuteka nyara, Upesi kwenye hizo nyara.
2 cNami nitawaita kuhani Uria, na Zekaria mwana wa Yeberekia kama mashahidi wangu waaminifu.” 3 dKisha nikaenda kwa nabii mke, naye akapata mimba, akazaa mwana. Kisha Bwana akaniambia, “Mwite huyo mtoto Maher-Shalal-Hash-Bazi. 4 eKabla mtoto hajaweza kusema ‘Baba yangu’ au ‘Mama yangu,’ utajiri wa Dameski na nyara za Samaria zitachukuliwa na mfalme wa Ashuru.” 5Bwana akasema nami tena: 6 f“Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya Shilo yatiririkayo taratibu
wakamfurahia Resini na mwana wa Remalia,
Copyright information for
SwhKC