Job 1:1-6

(Ayubu 1–2)

Ayubu Na Jamaa Yake

1 aKatika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu. 2 bAlikuwa na wana saba na binti watatu, 3 cnaye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.

4 dWanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao. 5 eWakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.

Jaribu La Kwanza La Ayubu

6 fSiku moja wana wa Mungu
Wana wa Mungu hapa ina maana malaika au viumbe vya mbinguni.
walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani
Shetani hapa ina maana ya mshtaki wa watakatifu.
naye akaja pamoja nao.
Copyright information for SwhKC