Job 18:11-16


11 aVitisho vimemtia hofu kila upande,
na adui zake humwandama kila hatua.

12 bJanga linamwonea shauku;
maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.

13 cNayo yatakula sehemu ya ngozi yake;
mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.

14 dAtang’olewa kutoka usalama wa hema lake,
na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.

15 eMoto utakaa katika hema lake;
moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.

16 fMizizi yake chini itakauka
na matawi yake juu yatanyauka.
Copyright information for SwhKC