Job 21:1-6

Ayubu Anajibu: Waovu Mara Nyingi Huenda Bila Kuadhibiwa

1Ndipo Ayubu akajibu:
2 a“Yasikilizeni maneno yangu kwa makini;
hii na iwe faraja mnayonipa mimi.

3 bNivumilieni ninapozungumza,
nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki.


4 c“Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu?
Kwa nini nisikose subira?

5 dNiangalieni mkastaajabu;
mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu.

6 eNinapowaza juu ya hili, ninaogopa,
nao mwili wangu unatetemeka.
Copyright information for SwhKC