Job 8:1-6
Bildadi Anasema: Yampasa Ayubu Atubu
1 aKisha Bildadi Mshuhi akajibu:2 b“Hata lini wewe utasema mambo kama haya?
Maneno yako ni kama upepo mkuu.
3 cJe, Mungu hupotosha hukumu?
Je, Mwenyezi hupotosha kile kilicho haki?
4 dWatoto wako walipomtenda dhambi,
aliwapa adhabu ya dhambi yao.
5 eLakini ukimtafuta Mungu,
nawe ukamsihi Mwenyezi,
6 fikiwa wewe ni safi na mnyofu,
hata sasa atainuka mwenyewe kwa niaba yako,
na kukurudisha katika mahali pako pa haki.
Copyright information for
SwhKC