John 10:1-6

Mchungaji Mwema

1 a“Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyang’anyi. 2 bYeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo. 3 cMlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi. 4 dAkiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake. 5 eLakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.” 6 fIsa alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.

Copyright information for SwhKC