John 18:2-7
2 aBasi Yuda, yule aliyemsaliti alipafahamu mahali hapo kwani Isa alikuwa akikutana humo na wanafunzi wake mara kwa mara. 3 bHivyo Yuda akaja bustanini. Aliongoza kikosi cha askari wa Kirumi, na baadhi ya maafisa kutoka kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Nao walikuwa wamechukua taa, mienge na silaha. 4 cIsa akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao akawauliza, “Mnamtafuta nani?” 5 dWao wakamjibu, “Isa Al-Nasiri.” Isa akawajibu, “Mimi ndiye.” Yuda, yule aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao. 6Isa alipowaambia, “Mimi ndiye,” walirudi nyuma na kuanguka chini! 7 eAkawauliza tena, “Mnamtafuta nani?” Nao wakamjibu, “Isa Al-Nasiri.”
Copyright information for
SwhKC