Luke 20:1-6
Swali Kuhusu Mamlaka Ya Isa
(Mathayo 21:23-27; Marko 11:27-33)
1 a bSiku moja, Isa alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia. 2 cWakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?” 3Akawajibu, “Nami nitawauliza swali. 4 dJe, ubatizo wa Yahya ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?” 5Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’ 6 eLakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yahya alikuwa nabii.”
Copyright information for
SwhKC