Mark 5:1-6

Isa Amponya Mtu Mwenye Pepo

(Mathayo 8:28-34; Luka 8:26-39)

1 aWakafika upande wa pili wa ziwa wakaingia katika nchi ya Wagerasi. 2 bIsa alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini akakutana naye. 3Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo. 4Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia. 5Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.

6Alipomwona Isa kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake.
Copyright information for SwhKC