Matthew 1:1-6

Kumbukumbu Za Ukoo Wa Isa Al-Masihi

(Luka 3:23-38)

1 aHabari za ukoo wa Isa Al-Masihi mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu:


2 bIbrahimu akamzaa Isaka,
Isaka akamzaa Yakobo,
Yakobo akawazaa Yuda na ndugu zake,

3 cYuda akawazaa Peresi na Zera, ambao mama yao alikuwa Tamari,
Peresi akamzaa Hesroni,
Hesroni akamzaa Aramu,

4 Aramu akamzaa Aminadabu,
Aminadabu akamzaa Nashoni,
Nashoni akamzaa Salmoni,

5 dSalmoni akamzaa Boazi, na mama yake Boazi alikuwa Rahabu,
Boazi akamzaa Obedi, ambaye mama yake alikuwa Ruthu,
Obedi akamzaa Yese,

6 eYese akamzaa Daudi ambaye alikuwa mfalme.

Daudi akamzaa Sulemani, ambaye mama yake ni yule aliyekuwa mke wa Uria.
Copyright information for SwhKC