Matthew 24:1-6
Kubomolewa Kwa Hekalu Kwatabiriwa
(Marko 13:1-2; Luka 21:5-6)
1 aIsa akatoka Hekaluni na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya Hekalu. 2 bNdipo Isa akawauliza, “Je, mnayaona haya yote? Amin, nawaambia, hakuna hata jiwe moja hapa litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”Ishara Za Nyakati Za Mwisho
(Marko 13:3-23; Luka 21:7-24)
3 cIsa alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamjia faraghani, wakamuuliza, “Tuambie, mambo haya yatatukia lini, nayo dalili ya kuja kwako na ya mwisho wa dunia ni gani?” 4 dIsa akawajibu, “Jihadharini, mtu yeyote asiwadanganye. 5 eKwa maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye Al-Masihi,’ ▼▼ Al-Masihi maana yake ni Masiya , yaani Aliyetiwa mafuta.
nao watawadanganya wengi. 6 gMtasikia habari za vita na matetesi ya vita. Angalieni msitishike, kwa maana haya hayana budi kutukia. Lakini ule mwisho bado.
Copyright information for
SwhKC