Numbers 11:25-29

25 aKisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Musa, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Musa na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.

26 bLakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini. 27Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Musa, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”

28 cYoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Musa tangu ujana wake, akajibu akasema, “Musa bwana wangu, wanyamazishe!”

29 dLakini Musa akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!”
Copyright information for SwhKC