Proverbs 19:5-10


5 aShahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa,
naye amwagaye uongo hataachwa huru.


6 bWengi hujipendekeza kwa mtawala
na kila mmoja ni rafiki wa mtu atoaye zawadi.


7 cMtu maskini huepukwa na ndugu zake wote:
Je, marafiki zake watamkwepa kiasi gani!
Ingawa huwafuata kwa kuwasihi,
hawapatikani popote.


8 dYeye apataye hekima huipenda nafsi yake mwenyewe,
yeye ahifadhiye ufahamu hustawi.


9 eShahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa,
naye amwagaye uongo ataangamia.


10 fHaistahili mpumbavu kuishi katika anasa,
itakuwa vibaya kiasi gani
kwa mtumwa kuwatawala wakuu.

Copyright information for SwhKC