Psalms 102:1-6

Maombi Ya Mtu Mwenye Taabu

(Maombi Ya Mtu Aliyechoka. Anapoteseka, Anapomimina Malalamiko Yake Kwa Bwana)


1 aEe Bwana, usikie maombi yangu,
kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.

2 bUsinifiche uso wako
ninapokuwa katika shida.
Unitegee sikio lako,
ninapoita, unijibu kwa upesi.


3 Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi,
mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.

4 cMoyo wangu umefifia na kunyauka kama jani,
ninasahau kula chakula changu.

5 dKwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu,
nimebakia ngozi na mifupa.

6 eNimekuwa kama bundi wa jangwani,
kama bundi kwenye magofu.
Copyright information for SwhKC