Psalms 104:1-6

Kumsifu Muumba


1 aEe nafsi yangu, umhimidi Bwana.

Ee Bwana Mwenyezi Mungu wangu, wewe ni mkuu sana,
umejivika utukufu na enzi.

2 bAmejifunika katika nuru kama vile kwa vazi,
amezitandaza mbingu kama hema

3 cna kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji.
Huyafanya mawingu kuwa gari lake,
na hupanda kwenye mbawa za upepo.

4 dHuzifanya pepo kuwa wajumbe
Au: malaika.
wake,
miali ya moto watumishi wake.


5 fAmeiweka dunia kwenye misingi yake,
haiwezi kamwe kuondoshwa.

6 gUliifunika kwa kilindi kama kwa vazi,
maji yalisimama juu ya milima.
Copyright information for SwhKC