Psalms 104:1-6
Kumsifu Muumba
1 aEe nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Ee Bwana Mwenyezi Mungu wangu, wewe ni mkuu sana,
umejivika utukufu na enzi.
2 bAmejifunika katika nuru kama vile kwa vazi,
amezitandaza mbingu kama hema
3 cna kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji.
Huyafanya mawingu kuwa gari lake,
na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 dHuzifanya pepo kuwa wajumbe ▼
▼ Au: malaika.
wake,miali ya moto watumishi wake.
5 fAmeiweka dunia kwenye misingi yake,
haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 gUliifunika kwa kilindi kama kwa vazi,
maji yalisimama juu ya milima.
Copyright information for
SwhKC