Psalms 115:3-8


3 aMungu wetu yuko mbinguni,
naye hufanya lolote limpendezalo.

4 bLakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu,
zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.

5 cZina vinywa, lakini haziwezi kusema,
zina macho, lakini haziwezi kuona;

6 zina masikio, lakini haziwezi kusikia,
zina pua, lakini haziwezi kunusa;

7 zina mikono, lakini haziwezi kupapasa,
zina miguu, lakini haziwezi kutembea;
wala koo zao haziwezi kutoa sauti.

8 dWale wanaozitengeneza watafanana nazo,
vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.

Copyright information for SwhKC