Psalms 19:1-6

Utukufu Wa Mungu Katika Uumbaji

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)


1 aMbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,
anga zahubiri kazi ya mikono yake.

2 bSiku baada ya siku zinatoa habari,
usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.

3 Hakuna msemo wala lugha,
ambapo sauti zao hazisikiki.

4 cSauti yao imeenea duniani pote,
nayo maneno yao yameenea
hadi miisho ya ulimwengu.

Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,

5 dlinafanana na bwana arusi
akitoka chumbani mwake,
kama shujaa afurahiavyo
kukamilisha kushindana kwake.

6 eHuchomoza upande mmoja wa mbingu,
na kufanya mzunguko wake
hadi upande mwingine.
Hakuna kilichojificha joto lake.

Copyright information for SwhKC