Psalms 22:1-6

Kilio Cha Uchungu Na Wimbo Wa Sifa

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Utenzi Wa Kulungu Wa Alfajiri. Zaburi ya Daudi)


1 aMungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa?
Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?

2 bEe Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu,
hata usiku, sinyamazi.


3 cHata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu;
wewe ni sifa ya Israeli.
Tafsiri zingine zinasema: uketiye juu ya sifa za Israeli.


4 eKwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao,
walikutumaini nawe ukawaokoa.

5 fWalikulilia wewe na ukawaokoa,
walikutegemea wewe nao hawakuaibika.


6 gMimi ni mnyoo wala si mwanadamu,
wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
Copyright information for SwhKC