Psalms 49:1-6
Upumbavu Wa Kutegemea Mali
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora)
1 aSikieni haya, enyi mataifa yote,
sikilizeni, ninyi wote mkaao dunia hii.
2 bWakubwa kwa wadogo,
matajiri na maskini pamoja:
3 cKinywa changu kitasema maneno ya hekima,
usemi wa moyo wangu utatoa ufahamu.
4 dNitatega sikio langu nisikilize mithali,
nitafafanua kitendawili kwa zeze:
5 eKwa nini niogope siku mbaya zinapokuja,
wakati wadanganyifu waovu wanaponizunguka,
6 fwale wanaotegemea mali zao
na kujivunia utajiri wao mwingi?
Copyright information for
SwhKC