Psalms 49:1-6

Upumbavu Wa Kutegemea Mali

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora)


1 aSikieni haya, enyi mataifa yote,
sikilizeni, ninyi wote mkaao dunia hii.

2 bWakubwa kwa wadogo,
matajiri na maskini pamoja:

3 cKinywa changu kitasema maneno ya hekima,
usemi wa moyo wangu utatoa ufahamu.

4 dNitatega sikio langu nisikilize mithali,
nitafafanua kitendawili kwa zeze:


5 eKwa nini niogope siku mbaya zinapokuja,
wakati wadanganyifu waovu wanaponizunguka,

6 fwale wanaotegemea mali zao
na kujivunia utajiri wao mwingi?
Copyright information for SwhKC