Psalms 51:1-6

Kuomba Msamaha

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi. Baada Ya Kukemewa Na Nabii Nathani Kwa Kuzini Na Bathsheba)


1 aEe Mungu, unihurumie,
kwa kadiri ya upendo wako usiokoma,
kwa kadiri ya huruma yako kuu,
uyafute makosa yangu.

2 bUnioshe na uovu wangu wote
na unitakase dhambi yangu.


3 cKwa maana ninajua makosa yangu,
na dhambi yangu iko mbele yangu daima.

4 dDhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi
na kufanya yaliyo mabaya machoni pako,
ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo,
na kuwa na haki utoapo hukumu.

5 eHakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi,
mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.

6 fHakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni,
ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.

Copyright information for SwhKC