a 2Sam 24:14; 12:13; Za 39:8; 86:15; 25:7; 119:88; 9:13; Neh 4:5; 9:27; Isa 63:7; Kol 2:14; 2Nya 6:23; Mdo 3:19
Psalms 51:1-6
Kuomba Msamaha
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi. Baada Ya Kukemewa Na Nabii Nathani Kwa Kuzini Na Bathsheba)
1 aEe Mungu, unihurumie,
kwa kadiri ya upendo wako usiokoma,
kwa kadiri ya huruma yako kuu,
uyafute makosa yangu.
2 bUnioshe na uovu wangu wote
na unitakase dhambi yangu.
3 cKwa maana ninajua makosa yangu,
na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
4 dDhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi
na kufanya yaliyo mabaya machoni pako,
ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo,
na kuwa na haki utoapo hukumu.
5 eHakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi,
mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
6 fHakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni,
ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.
Copyright information for
SwhKC