Psalms 51:2-7


2 aUnioshe na uovu wangu wote
na unitakase dhambi yangu.


3 bKwa maana ninajua makosa yangu,
na dhambi yangu iko mbele yangu daima.

4 cDhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi
na kufanya yaliyo mabaya machoni pako,
ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo,
na kuwa na haki utoapo hukumu.

5 dHakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi,
mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.

6 eHakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni,
ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.


7 fNioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi,
unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
Copyright information for SwhKC