Psalms 57:1-3

Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Usiharibu! Utenzi Wa Daudi. Baada Ya Kumponyoka Sauli Pangoni)


1 aUnihurumie, Ee Mungu, unihurumie,
kwa maana nafsi yangu inakukimbilia.
Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia
mpaka maafa yapite.


2 bNamlilia Mungu Aliye Juu Sana,
Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.

3 cHutumana kutoka mbinguni na kuniokoa,
akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali;
Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.

Copyright information for SwhKC