Psalms 73:1-6
(Zaburi 73–89)
Haki Ya Mungu
(Zaburi Ya Asafu)
1 aHakika Mungu ni mwema kwa Israeli,
kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 bBali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza;
nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 cKwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna
nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Wao hawana taabu, ▼
▼ Tafsiri nyingine zinasema: hawana maumivu katika kufa kwao.
miili yao ina afya na nguvu.
5 eHawapati shida zinazowataabisha watu wengine,
wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 fKwa hiyo kiburi ni mkufu wao,
wamejivika jeuri.
Copyright information for
SwhKC