Psalms 73:1-6

(Zaburi 73–89)

Haki Ya Mungu

(Zaburi Ya Asafu)


1 aHakika Mungu ni mwema kwa Israeli,
kwa wale ambao mioyo yao ni safi.


2 bBali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza;
nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.

3 cKwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna
nilipoona kufanikiwa kwa waovu.


4 Wao hawana taabu,
Tafsiri nyingine zinasema: hawana maumivu katika kufa kwao.

miili yao ina afya na nguvu.

5 eHawapati shida zinazowataabisha watu wengine,
wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.

6 fKwa hiyo kiburi ni mkufu wao,
wamejivika jeuri.
Copyright information for SwhKC