Mark 1:12-13
Majaribu Ya Yesu
(Mathayo 4:1-11; Luka 4:1-13)
12Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani, 13naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
Copyright information for
SwhNeno