‏ Mark 3:13-19

Yesu Achagua Mitume Kumi Na Wawili

(Mathayo 10:1-4; Luka 6:12-16)

13Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia. 14Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri 15na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu. 16Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro); 17Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo); 18Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo, 19na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
Copyright information for SwhNeno