Psalms 131
Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. 1Moyo wangu hauna kiburi, Ee Bwana,macho yangu hayajivuni;
sijishughulishi na mambo makuu kunizidi
wala mambo ya ajabu mno kwangu.
2Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya
ndivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.
3Ee Israeli, mtumaini Bwana
tangu sasa na hata milele.
Copyright information for
SwhNeno