‏ Psalms 131

Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1Moyo wangu hauna kiburi, Ee Bwana,
macho yangu hayajivuni;
sijishughulishi na mambo makuu kunizidi
wala mambo ya ajabu mno kwangu.
2Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya
ndivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.

3Ee Israeli, mtumaini Bwana
tangu sasa na hata milele.
Copyright information for SwhNeno