Luke 3:21-22
Kubatizwa Kwa Bwana Yesu
(Mathayo 3:13-17; Marko 1:9-11)
21Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka. 22Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
Copyright information for
SwhNeno