‏ Psalms 57:7-11

7Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti;
nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8Amka, nafsi yangu!
Amka, kinubi na zeze!
Nitayaamsha mapambazuko.

9Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa;
nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni,
uaminifu wako unazifikia anga.

11Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni,
utukufu wako na uwe duniani pote.
Copyright information for SwhNeno